Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » , , » AMANDA WA BONGO MOVIE AMTAMBULISHA "BWANA MISOSI" KWA WAZAZI WAKE

AMANDA WA BONGO MOVIE AMTAMBULISHA "BWANA MISOSI" KWA WAZAZI WAKE

tangazo

MWIGIZAJI wa sinema za Kibongo, Tamrina Mohamed ‘Amanda’ amemtambulisha mume wake mtarajiwa, staa wa Bongo Fleva, Joseph Rushau ‘Bwana Misosi’ kwa wazazi wake.

Tukio hilo lilichukua nafasi mwishoni mwa wiki iliyopita pande za Msasani Beach, jijini Dar wakati mwigizaji huyo alipokuwa akiadhimisha siku yake ya kuzaliwa, ndipo alipotumia nafasi hiyo kumtambulisha Bwana Misosi kwa mama yake mzazi na mjomba wake.

“Kula keki na kunywa shampeni pamoja na mama yangu, mjomba, mama Dotnata na wageni waalikwa ni ishara tosha kwamba Misosi umekubalika katika familia yetu, jisikie uko nyumbani,” alisikika Amanda.


Katika shughuli hiyo, Amanda alimuandalia mpenzi wake huyo ambaye ni mwanamuziki keki maalum yenye muonekano wa gitaa kama ishara ya upendo kwake.

TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger