Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » , » "SIJAWAHI GAWA PENZI LANGU KWA SLIM"- BABY MADAHA.

"SIJAWAHI GAWA PENZI LANGU KWA SLIM"- BABY MADAHA.

tangazo
MWANADADA mwigizaji wa filamu na mwanamuziki Baby Madaha amekanusha kuwa na uhusiano na mwigizaji mwenzake wa filamu Slim baada ya habari za uhusiano wao kuvuma na kusababisha ugomvi na mzazi mwenzake Slim ambaye pia ni rafiki yake Baby Madaha, msanii huyo amedai kuwa hana uhusiano wa kimapenzi na Slim bali alimshirikisha katika video ya wimbo wake tu.

baby Madaha
Baby Madaha
“Maneno mengi yanasemwa lakini ukweli ni kwamba sina uhusiano na Slim bali kilichotokea nilikuwa natengeneza video yangu ya muziki na nilihitaji kumpata mwanaume mwenye muonekano mzuri na mrefu kama Slim kwa hiyo kishemeji shemeji nikafanya naye kazi kama msanii mwenzangu na shemeji yangu,”anasema Baby Madaha.

Lakini jambo la ajabu rafiki yake ambaye ndio mzazi mwenzake na Slim alikasirika na kutengeneza bifu akijua anatoka naye, Baby Madaha akisema lakini pia baadae aligundua kuwa tayari rafiki yake huyo alikuwa ametengana na Slim, Madaha anasema kuwa yeye hana mwanaume yoyote na hataki mwanaume zaidi ya maisha yake ya Single
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger