Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » , » PROFESA JAY AZUSHIWA KIFO....

PROFESA JAY AZUSHIWA KIFO....

tangazo


Kuna habari za uzushi zimesambaa leo kuwa rapper Joseph Haule aka Profesa Jay amefariki dunia ambazo kwa mujibu wake mwenyewe Profesa zimemshtua mama yake kwa kiasi kikubwa.


Taarifa hizo za uzushi zimedai kuwa Profesa Jay alianguka na kuzimia na wengine kudai amefariki.

Kupitia mtandao wa Twitter, Profesa Jay amezikanusha taarifa hizo kwa kuandika, “Jamani eeeh mimi ni mzima wa afya njema hao wanaozusha kuwa nimekufa wataanza wenyewe. Mi niko fresh mpaka natamani kujiteka.”

“Watu hawana kazi za kufanya kila siku kuwaombea wenzao mabaya tu maisha sijui yamewashinda wamekalia uzushi tu. Leo zamu yangu nimepigiwa simu mpaka nimeshangaa kumbe watu wanataka kuhakikisha mzee washindwe na walegee,” aliongeza.

“Imemshtua sana mama yangu maana alinisikia nilipokuwa nikioongea na moja ya simu zilizokuwa zinanipa ripoti hii.”
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger