Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » , » TASWIRA ZA WAOMBOLEZAJI NYUMBANI KWA MAREHEMU OMAR OMAR TEMEKE-MIKOROSHINI JIJINI DAR

TASWIRA ZA WAOMBOLEZAJI NYUMBANI KWA MAREHEMU OMAR OMAR TEMEKE-MIKOROSHINI JIJINI DAR

tangazo

Ndugu na jamaa wakiwa na majonzi msibani kwa marehemu Omar Omar, Temeke-Mikoroshini jijini Dar.

Marehemu Omar Omar enzi za uhai wake.

Dada wa marehemu (hakufahamika jina lake mara moja) akiwasiliana na ndugu wengine ambao hawapo msibani.

Mwanamuziki wa kizazi kipya, Dully Sykes, mwenye T-shirt  ya mistari (nyuma katikati) akibadilishana mawazo na wazee msibani hapo.
Meneja wa marehemu, Bonga Ticha (kushoto) akiwa na meneja wa kundi la muziki la Wanaume Family, Mkubwa Fella.

Baadhi ya wasanii wa muziki wa kizazi kipya na mameneja wao wakiwa msibani hapo.
----------------------
WAOMBOLEZAJI mbalimbali wakiwemo wasanii wa muziki wa kizazi kipya, leo wamekusanyika nyumbani kwa mwanamuziki mkongwe wa miondoko ya mnanda, Omar Omar Mfungilo, aliyefariki dunia usiku wa kuamkia leo nyumbani kwao Temeke-Mikoroshini, Dar es Salaam. Kwa mujibu wa baba mdogo wa marehemu, mzee Yusufu Ally Mfungilo, marehemu Omar anatarajiwa kuzikwa kesho saa saba mchana huko Temeke.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger