Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » HII NDIO ASILIMIA YA WATANZANIA WASIOTAZAMA TV JIJINI DAR TANGU MFUMO WA DIGITALI ULIPOANZA

HII NDIO ASILIMIA YA WATANZANIA WASIOTAZAMA TV JIJINI DAR TANGU MFUMO WA DIGITALI ULIPOANZA

tangazo

Tulikua na uhakika kwamba ni idadi ndogo ya Watanzania waliofanikiwa kununua na kuvitumia vinga’muzi toka mfumo wa digital uanze kutumika Tanzania lakini hatukuwahi kupata ni asilimia ngapi ya watu ambao hawatazami Tv kutokana na kukosa vinga’muzi.

Taarifa imetufikia kwamba utafiti wa haraka uliofanywa na umoja wa wamiliki wa vyombo vya habari MOAT umeonyesha kwamba kwa Dar es salaam pekee, ni zaidi ya asilimia 75 ya Watanzania haitazami channel za TV za nyumbani toka kuzimwa kwa mitambo ya analog ndio maana umoja huo bado umeendelea na msimamo wa kuitaka serikali kuangalia upya uwezekano wa kurudisha matangazo ya analog kwanza.

Haya ni maelezo ya mwenyekiti wa MOAT Reginald Mengi: “Watanzania wapewe muda kujiandaa ili kutoka analog kwenda digital ifanyike vizuri na kwa mafanikio makubwa, pendekezo letu lilikua ni kwamba analog na digital ziende sambamba mpaka tufike mahali tuone kwamba watu wengi kama sio wote wana vyombo vya kuwawezesha kwenda digital, hilo lifanyike kabla ya tarehe 17 june 2015 ambayo ndio siku ya mwisho ya kutumia analog”

milardayo
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger