Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » KUNDI LA CAMP MULLA LAZIDI KUPASUKA....

KUNDI LA CAMP MULLA LAZIDI KUPASUKA....

tangazo
Hivi karibuni tuliandika habari kuhusu kundi linaloundwa na vijana wanne wenye vipaji kutoka Kenya linalofahamika kama Camp Mulla kumpoteza member mmoja ambaye ndio aliyekuwa msichana pekee katika kundi aitwaye Miss Karun.


Mwanzo ulianza kama uvumi kuwa Miss Karun amepigwa chini na kundi hilo na nafasi yake kuchukuliwa na msichana mwingine aitwaye Tiri, lakini habari mpya habari zilizothibitishwa Kupitia mtandao wa kituo kikubwa Africa Kusini Channel O, zinasema Miss Karun ameamua kujiondoa kwenye kundi kwaajili ya maandalizi ya kujiunga na chuo. 
 

Miss Karun anategemewa kwenda masomoni nchini Marekani mwezi August mwaka huu, lakini ataendelea kufanya muziki kama solo.

camp m

Kama vile haitoshi, kwa mujibu wa mtandao huo member mwingine aitwaye Thee Mc Africa zamani alifahamika kama Taio Tripper naye amejitoa katika kundi hilo na ataendelea kufanya muziki kama solo. 
 

Kundi hilo lilianzishwa mwaka 2009 likiwa na members wanne, Kwa sasa limebaki na members wawili wa mwanzo pamoja na msanii mpya wa kike aitwaye Tiri.

TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger