Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » NAIBU SPIKA AAPA KUTOMWADHIBU MBUNGE YEYOTE KWA MADAI KWAMBA AMECHOKA KUITWA ZEZETA

NAIBU SPIKA AAPA KUTOMWADHIBU MBUNGE YEYOTE KWA MADAI KWAMBA AMECHOKA KUITWA ZEZETA

tangazo

Naibu Spika wa Bunge,Ndugu Job Ndugai amesema kuwa kuanzia sasa hatamwadhibu Mbunge yeyote anayeleta vurugu Bungeni kwakuwa amechoka lawama. 

 Akihojiwa na Redio One Stereo katika kipindi cha Kumepambazuka leo asubuhi ,Ndugai amesema kuwa yeye amechoka kuitwa mzembe,zezeta na goigoi na vyombo vya habari.

Ndugai amesema kuwa hata kwa Wabunge waliosababisha tafrani Bungeni jana kiasi cha kuchana Nyaraka za Bunge,hawatachukuliwa hatua yoyote.


 "Kila Mbunge anayeadhibiwa na Kiti cha Spika anaonekana Shujaa. Sisi tunamuona mtovu wa nidhamu,wananchi wanamuona shujaa.Siko tayari tena kwa hilo".alisema Ndugai

Kuhusu uandalizi wa Bajeti ya Kambi Rasmi ya Upinzani na kama hupitiwa kabla ya kusomwa Bungeni,Ndugai amesema kuwa Bajeti hizo zinapaswa kujadili mafungu ya Bajeti husika ya Serikali na si vinginevyo. 


"Kwanza hawa wenzetu wanatoka na Bajeti zao nyumbani moja kwa moja na kuja kuzisoma pale.Hawapaswi kutunga za kwao.Wanatakiwa kujadili mafungu ya Bajeti ya Wizara husika tu. Wakati mwingine mtu mmoja anajiandikia tu Bajeti ya Upinzani wenzake hawawezi kumkana Bungeni" alisema kwa hasira Ndugai.

Alipoulizwa kuhusu kutenda haki kwa kuwaadhibu na Wabunge waCCM,Ndugai alikwepa na kuanza kufoka kuhusu Wabunge wa CHADEMA kuwa hawana nidhamu na hatowagusa tena. ‘Watanzania si ndivyo watakavyo….sawa,na sisi tutawaacha ili wasiwe mashujaa!’ alisisitiza Ndugai. 


Credit: JF
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger