Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » MWANAFUNZI AJIUA BAADA YA KUBAKWA HUKO SUMBAWANGA

MWANAFUNZI AJIUA BAADA YA KUBAKWA HUKO SUMBAWANGA

tangazo

Mwanafunzi wa kidato cha nne, Flora Athanas (18) wa sekondari Mzindakaya wilayani hapa amejiua kwa sumu ya panya, baada ya kubakwa na mtu asiyefahamika.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda, alisema jana kuwa mwanafunzi huyo alibakwa usiku wa kuamkia Jumanne yeye na mwenzake, katika chumba walimopanga, kutokana na kukosekana kwa mabweni katika shule hiyo.

Kwa mujibu wa Kamanda Mwaruanda, siku hiyo Flora alikuwa na wanafunzi wenzake watatu, akiishi nao katika chumba hicho.

Inadaiwa usiku mtu asiyefahamika, alivamia nyumba walimopanga, akafunga vyumba vya wanafunzi wengine na kuingia chumba cha akina Flora akiwa na kisu na kuwatishia kuwa atakayepiga kelele atamuua kwa kisu.

Kutokana na tishio hilo, inadaiwa wanafunzi hao walikaa kimya na mvamizi huyo kumbaka Flora na mwenzake na kumwacha mwingine na kukimbilia kusikojulikana. 

Asubuhi siku hiyo, Flora aliamka, akatoroka na kwenda katika   duka kijijini hapo na kununua sumu ya panya.

Inadaiwa aliondoka na sumu hiyo kwenda porini nje kidogo ya kijiji cha Kaengesa, ambako hufanyika mnada wa hadhara na kukatisha maisha  yake kwa sumu hiyo.
 

“Uchunguzi wa awali wa Polisi unaonesha kuwa kifo hicho  kimesababishwa na hasira ya msichana huyo,“ alisema Kamanda Mwaruanda.

Aliongeza kuwa mwanafunzi mwenzake aliyebakwa pamoja naye, alifikishwa katika kituo cha afya Kaengesa, na kufanyiwa uchunguzi wa kitabibu kuthibitisha kubakwa kwake.
 

Katika kituo hicho, ndiko pia mwili wa marehemu ulipelekwa kwa uchunguzi na kuthibitika kuwa chanzo cha kifo hicho ni sumu ya panya.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger