Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » "WASANII WENGI WA BONGO MOVIE NI OMBA OMBA...ACCOUNT ZAO HAZINA KITU"... BATULI

"WASANII WENGI WA BONGO MOVIE NI OMBA OMBA...ACCOUNT ZAO HAZINA KITU"... BATULI

tangazo

Batulli  ambaye  ni mmoja wa waigizaji wa kike warembo nchini na ambaye jina lake halisi ni Yobnesh Yussuph aka Nesh, amefunguka kwenye Twitter kuwa licha ya soko la movie kupanuka, waigizaji wengi hawana kitu.

 
“Wasanii wengi wa filamu huwa tunaamka asubuhi hata hatujui tutakula nini. Accounts zetu hazina kitu wakati tuna film nyingi sana sokoni,” ametweet.

 
“Wenzetu huamka na mipango kamili ya siku iliyopo lakini wasanii wa film huwa tunaamka huku tukiwaza ni nani wa kumpiga kibomu siku iende. 



"Jina kubwa umejibana umepata gari yako 1 tena used, siku ikiipeleka garage unashinda na wewe huko huko garage kazi zote unasimamisha #Huruma.

Batulli ameilalamikia pia mikataba mibovu iliyopo kwenye filamu.

 
“Mikataba ya kazi za film Tanzania ukiisoma unaweza ukajuta kwanini uliamua kuwa muigizaji, unauza movie yako na haki miliki kwa miaka 50. 


"Hakuna anaependa ndio maana tunalia na serikali mikataba ibadilishwe tupewe kipaumbele movie niuze leo nimiliki baada ya 50 yrs? 


"Unapoenda kuuza kazi halafu tajiri anakupangia bei ya kuinunua pasipo kuangalia gharama ulizotumia ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu.”
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger