Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » Basi la Al Sayeed lapata ajali na kuua watu sita....Hii ni video ya tukio hilo

Basi la Al Sayeed lapata ajali na kuua watu sita....Hii ni video ya tukio hilo

tangazo
 
Watu sita wamefariki dunia na wengine 34 kujeruhiwa katika ajali ya barabarani iliyotokea eneo la Chinangali wilayani Chamwino mkoani Dodoma baada ya basi la kampuni ya Al Sayeed lililokuwa likitokea jijini Dar-Es-Salaam kwenda Dodoma kugongana uso kwa uso na lori la mizigo lililobeba shehena ya mahindi likitokea Dodoma kwenda Dar es salaam.
 

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Dodoma Mrakibu Mwandamizi Damas Nyanda amesema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva wa basi hilo lenye namba za usajili T 433 BLR aina ya Youtong ambaye alishindwa kulimudu na kuacha njia na kulivaa lori aina ya Layland Daf lenye namba za usajili T 102 CGR likiwa na tela lenye namba za T 928 na kusababisha watu watano kufariki papo hapo.
 
ITV ilifika katika eneo la tukio na kuzungumza na baadhi ya mashuhuda wa ajali hiyo na wamelalamikia uhaba wa vyombo vya uokoaji ambapo wamesema kama vyombo vya uokoaji vingefika kwa wakati huenda watu wote wanne waliofariki kwenye lori wangeokolewa.
 
Nao baadhi ya majeruhi waliolazwa katika hosipitali ya rufaa ya Dodoma wamesema kabla ya kutokea kwa ajali hiyo dereva wa basi hilo alikuwa katika mwendo kasi na baada ya kuliona lori hilo alifunga breki za ghafla na kusababisha basi hilo kulivaa lori hilo huku mganga mfawidhi wa hosipitali hiyo Dk Mzee Nasoro akasema walipokea majeruhi 20 na mmoja kati yao amefariki dunia
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger