Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » Tishio jingine kubwa la Ugaidi nchini Kenya....Marekani yatoa angalizo kwa raia wake waishio Kenya kuwa tayari kwa lolote

Tishio jingine kubwa la Ugaidi nchini Kenya....Marekani yatoa angalizo kwa raia wake waishio Kenya kuwa tayari kwa lolote

tangazo
SIKU chache baada ya kikundi cha Al Shabaab kudaiwa kuteka Jengo la Westgate nchini Kenya na kuua watu kadhaa na wengine kujeruhiwa wasiwasi wa magaidi kulipua tena nchi hiyo umetanda.
 
Tayari Marekani imetoa angalizo kwa Kenya kuhusu uvamizi huo na kuitaka isibeze kuchukua tahadhari kama ilivyofanya kwa tukio la Westgate na kusababisha madhara makubwa kwa wananchi.
 
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa hivi karibuni na Baraza la Ushauri la Usalama wa Nje la Marekani ni kwamba kuna uwezekano mkubwa wa kutokea tena kwa shambulizi la ugaidi nchini Kenya.
 
Marekani imesema shambulio hilo litafanywa na kundi jipya la wanamgambo wa Kenya la Al Hijra ambalo linashirikiana na Al Shabaab na lengo lake ni kuharibu maeneo nyeti.
 
Kutokana na hali hiyo, Serikali ya Marekani imewataka raia wake kuwa makini wakati wanapokuwa kwenye maeneo ya umma katika miji ya Nairobi na Mombasa.
 
Tahadhari hiyo imekuja ikiwa ni siku kadhaa baada ya Al Shabaab kuishambulia Kenya  mwaka  huu  na Uganda mwaka 2010 na kusababisha vifo vya watu 77 ambao walikuwa wanaangalia mchezo wa mpira kwa njia ya televisheni.
 
Tukio la Westgate lilisababisha Umoja wa Mataifa (UN), Uingereza, Marekani na mataifa mengine makubwa kuelekeza masikio nchini Kenya kutokana na kushtushwa na shambulio hilo.

-Gazeti  la  Jambo  leo
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger