Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » CHADEMA YAFUNGUKA KUHUSU KAULI ZA NAPE NNAUYE KWAMBA KIKO MBIONI KUVUNIKA KWA "UBAGUZI"

CHADEMA YAFUNGUKA KUHUSU KAULI ZA NAPE NNAUYE KWAMBA KIKO MBIONI KUVUNIKA KWA "UBAGUZI"

tangazo

Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA, kimesema kuwa kauli iliyotolewa na Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi CCM, NAPE NNAUYE, kuwa chama hicho kitakufa kutokana na kuwa na Sumu ya Ubaguzi, haina ukweli wowote, na kumtaka kiongozi huyo kutafakari zaidi kauli hiyo kwa maslahi ya Chama chake.
 
Mkurugenzi wa Sera na Mafunzo wa CHADEMA, BENSON KIGAILA, amesema CHADEMA hakiwezi kufa kwa dhana iliyozungumzwa na NAPE, na badala yake Chama hicho Tawala ndicho kinachoweza kufa kutokana na kukabiliwa, na changamoto nyingi ikiwemo ufisadi.

 
Katika Hatua nyingine CHADEMA kimemtaka Naibu Katibu wa CCM, MWIGULU NCHEMBA, kutoa ushahidi wa kauli aliyoitoa hivi karibuni, kuwa Chama hicho kimekuwa kikipanga mipango ya mauaji na kubanisha kuwa kauli hiyo, imelenga kulidhalilisha jeshi la Polisi na Idara ya Usalama wa Taifa
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger