Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » , » LULU MICHAEL AKATAA KUFANYIWA "SHEREHE" YA KUPONGEZWA KUINGIA URAIANI

LULU MICHAEL AKATAA KUFANYIWA "SHEREHE" YA KUPONGEZWA KUINGIA URAIANI

tangazo


January 29 2013 ndio msajili alithibitisha kwamba mwigizaji Lulu ametimiza masharti yote ya dhamana juu ya kesi inayomkabili ya kuua bila kukusudia na hivyo  kumwachia  kwa dhamana.....
 
Lulu na mama yake mzazi wote kwa pamoja waliangua vilio baada ya dhamana yao kukamilika wakati wakiwa nje ya Mahakama kabla ya kuondoka na Lulu kuingia uraiani.

Kabla  ya dhamana  hiyo kulikwa  na  tetesi  kwamba  Lulu angefanyiwa  sherehe kubwa  ya  kupongezwa  kuja uraiani.

Kwa mujibu wa ndugu yake  wa karibu, Lulu amegoma  kufanyiwa sherehe  na  badala  yake jana aliwaomba  watanzania  wamuombee  kwa  mungu  maana  kesi bado inaendelea.....
 
 “Nawashukuru watu wote na nilikua naomba watu waendelee kuniombea sababu hii ni dhamana tu lakini kesi bado ina safari ndefu… nawashukuru wale wote waliokua na mimi kwa hali yeyote ile na zaidi zaidi namshukuru sana Mwenyezi Mungu”....LULU
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger