Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » , » MBUNGE WA KINONDONI AAHIDI KUISAIDIA FAMILIA YA SAJUKI

MBUNGE WA KINONDONI AAHIDI KUISAIDIA FAMILIA YA SAJUKI

tangazo

Kutokana na hali ya majonzi na masikitiko makubwa kwenye familia ya  marehemu Sajuki mbunge wa Kinondoni Iddi Azam ameahidi kuisaidia kwa hali na mali familia aliyoiacha marehemu Sajuki

Ahadi hizo alizisema juzi wakati alipofika nyumbani kwa marehemu kwa lengo la kutoa pole na salamu za rambirambi kwenye familia hiyo

Azam alisema kuwa anadeni kubwa kwenye familia hiyo pamoja na  mtoto aliyeachwa na marehemu, hivyo ni wajibu wake kumsaidia kadri ya uwezo wake

"Kila mtu anaiona hali ya Wastara sasa ilivyo basi sisi tulio baki tuwe kama Sajuki, kwani mapenzi walio kuwa nayo ni mfano wa kuigwa kwetu, hivyo nina jukumu la kuisaidia familia hii" alisema Azam

Aliongezea kuwa ni jukumu la kila mmoja wao kumuenzi marehemu Sajuki kwa vitendo Sajuki anazikwa leo katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger