Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA ST JOHNS WAANDAMANA KUPINGA KUBAKWA NA KUIBIWA CHUONI

WANAFUNZI WA CHUO KIKUU CHA ST JOHNS WAANDAMANA KUPINGA KUBAKWA NA KUIBIWA CHUONI

tangazo

Wanafunzi wakiwa na mabango leo mjini dodoma.
ZAIDI ya wanafunzi 4000 wa Chuo Kikuu cha St. John’s kilichopo mjini DODOMA  wameandamana wakililalamikia Jeshi la Polisi Nchini kwa kushindwa kuthibiti vitendo vya matukio ya ubakaji na kulawitiwa yanayofanyika chuoni hapo.

Wanafunzi hao ambao waliandamana umbali wa kilomita tatu leo kutoka chuo kilipo na kuishia viwanja vya Mwalimu Nyerere walidai wanalenga kufikisha ujumbe kwa jamii kutambua vitendo vya kikatili vinavyofanyika chuoni hapo.
Maandamano hayo ambayo yalikuwa yakisindikizwa na
Polisi wa kikosi cha kutuliza ghasia, yalipita katika mitaa mbalimbali ya Manispaa ya Dodoma.

Waandamanaji hao ambao mbali na kuimba nyimbo za kulilaumu Jeshi la Polisi kwa kushindwa kuthibiti vitendo hivyo, pia mabango waliyokuwa wamebeba yalikuwa yakililaumu jeshi hilo.
Askari jeshi la polisi wakijariobu kuwazuia wanafunzi leo mjini dodoma
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger