Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » NDOA YA AUNT EZEKIEL YAWEWESEKA.....

NDOA YA AUNT EZEKIEL YAWEWESEKA.....

tangazo

KUMEKUWEPO na vijineno vya chinichini kuwa eti ndoa ya msanii maarufu wa filamu Bongo, Aunt Ezekiel aliyofunga hivi karibuni na Sunday Demonte haipo na wabaya wake wamekuwa wakieneza taarifa hizo kwa kasi ya ajabu.
 
Wakizungumza na gazeti hili kwa nyakati tofauti, watu waliodai ni mashosti wa karibu wa staa huyo walisema wamebaini dalili za wazi kuwa ndoa yake imeyeyuka.

“Mimi ndiyo nawaambia sasa, kama mlikuwa hamjui ndoa ya Aunt haipo. Fuatilieni mtabaini ukweli wa hiki ninachowaambia.


“Nyie si mjiulize mbona tangu amerudi kutoka Dubai hajaenda tena kumfuata huyo mumewe? Si alisema amekuja kuweka mambo yake sawa kisha anakwenda kuifurahia ndoa yake, kiko wapi sasa?” alihoji mmoja wa wanyetishaji hao aliyeomba jina lake lisiandikwe gazetini.


Mwingine aliyekuwa mmoja wa waliofanikisha ndoa ya Aunt kwa kiasi kikubwa ambaye naye aliomba jina lake liwekwe kapuni alisema: 

“Hata mimi nina mashaka na hii ndoa ya huyu mwenzetu, lakini iwe imevunjika, haijavunjika sisi haituhusu, kila mtu ana maisha yake bwana.”


Katika kujua ukweli wa madai haya, mwandishi wetu alimtafuta Aunt na alipotakiwa kulizungumzia hilo alisema:


“Tuna mipango yetu mimi na familia ndiyo maana Sunday yupo Dubai na mimi huku. Sipendi kuongelea mambo ya ndoa yangu magazetini lakini kwa kifupi ipo sawa.”


GLOBAL
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger