Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » Papa Benedikto wa 16 ang’atuka rasmi huku mchakato wa kumchagua Papa mpya ukianza kesho

Papa Benedikto wa 16 ang’atuka rasmi huku mchakato wa kumchagua Papa mpya ukianza kesho

tangazo


Papa Emeritus .


Papa Benedikto wa 16 amejiuzulu rasmi leo kama kiongozi wa kanisa katoliki duniani ambapo katika hotuba yake ya mwisho kwa umati wa watu zaidi ya laki moja na nusu waliokusanyika katika uwanja wa Mtakatifu Petro, Benedikto wa 16 ambaye ni mzaliwa wa Ujerumani amezungumzia changamoto zilizolikumba kanisa wakati akiwa kiongozi wake, na kusema kuwa kuna wakati ilionekana kwake kama Mungu amesinzia. 

Hata hivyo, ameongeza kuwa mara zote alifahamu kuwa Mungu ndiye nahodha wa meli ya kanisa katolik, na kwamba kamwe asingeiacha meli hiyo izame. 

Kesho Siku ya Ijumaa makardinali wataanza mchakato wa kumchagua papa mpya. 

Kuanzia sasa Benedikti wa 16 atajulikana kama Papa Emeritus na atahamia katika chumba cha kitawa mjini Vatikani mwezi Aprili.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger