Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » IDADI YA WALIO UAWA NCHINI KENYA IMEFIKA 22....UHURU KENYATTA BADO ANAONGOZA

IDADI YA WALIO UAWA NCHINI KENYA IMEFIKA 22....UHURU KENYATTA BADO ANAONGOZA

tangazo
Kura zikihesabiwa kwenye kituo kilichopo Viwanja vya Kibera Social, jijini Nairobi baada ya wananchi wa Kenya kupiga kura katika uchaguzi mkuu wa nchi hiyo jana. Picha na AFP 
------------
Matokeo ya awali ya uchaguzi mkuu nchini Kenya yanaonyesha kuwa Uhuru Kenyatta, mtoto wa Rais wa Kwanza wa Kenya, Mzee Jomo Kenyatta anaongoza, huku akifuatiwa kwa karibu na aliyekuwa Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Raila Odinga.


Kama alivyo Uhuru, Raila pia ni mtoto wa mmoja wa waasisi wa taifa la Kenya, ambaye alikuwa Makamu wa Mzee Kenyatta, Jaramong Oginga Odinga.
Waliokufa wafikia 22

Wapema watu 22 wakiwamo askari polisi tisa waliripotiwa kuuwawa baada ya kuvamiwa na kikundi cha watu zaidi ya 200 huko Mombasa na Kilifi saa chache kabla ya Wakenya kuanza kupiga kura jana.

Saa chache kabla ya uchaguzi huo, askari polisi tisa waliuawa katika mashambulizi yaliyotokea kwenye miji ya Mombasa, Kilifi na Kwale na kuacha wavamizi wapatao 10 na raia wa kawaida watatu pia wakifariki.

Baada ya vifo hivyo, serikali ilipeleka vikosi vya askari kutoka Mariakani Barracks kwenda kutuliza ghasia hizo wakati kundi lingine la askari lilitoka Nyali Barracks kwa ajili ya kuweka doria katika miji ya Mombasa na North Coast.

Taarifa zilizopatikana baadaye jana zilisema kuwa kwenye mji wa Mombasa askari polisi wanne waliuawa na watu zaidi ya 100 waliovamia kituo cha kura cha Miritini.

Polisi pia ilithibitisha kuuawa kwa watu saba katika mapigano hayo huku na wengine kadhaa kutiwa nguvuni.

Wavamizi wengine waliuawa katika miji ya Kisauni na Kilifi huku polisi wanne wakiuawa Chumani na mmoja huko Chonyi huku watu watatu wakiuawa kwa kupigwa risasi.

Mwanachi
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger