Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » KANISA LA MASHOGA LAZINDULIWA TENA...

KANISA LA MASHOGA LAZINDULIWA TENA...

tangazo
Ikiwa ni miezi mitatu tu imepita toka nchi nyingine ambayo ni maarufu Afrika (Kenya) kukumbwa na headlines za kutosha kuhusu raia wake wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja kupeana tuzo hadharani na kufanya sherehe, leo tena headlines zimehamia Nigeria.

Ndani ya miaka mitano iliyopita huko Nigeria kulikua na Kanisa ambalo lina waumini wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja tu liitwalo House of Rainbow lakini Kanisa hilo lilipotea baada ya kushambuliwa na wakazi wa Lagos ambao hawapendezwi na ishu za ushoga na usagaji.

Tarehe 3 March 2013 Mtandao maarufu wa Nigeria wa TFJ umeripoti kwamba kanisa hilo limerejea tena kwa kishindo na kuendelea na huduma zake.


Ni kanisa ambalo mwanzilishi wake ni mchungaji Mnigeria ambae ni shoga Rowland Jide Macaulay na imefahamika sasa hivi kwamba kanisa hilo lipo Ghana na Malawi, France, Netherlands, Cote d’Ivoire na Sierra-Leone.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger