tangazo
Kiongozi mkuu wa kundi la al-Qaeda ameuawa nchini Mali. Taarifa hizi zimethibitishwa na Rais wa Chad, Idriss Deby Alisema kuwa majeshi ya nchi yalimuua Abdelhamid Abou Zeid, wakati wa makabiliano yaliyotokea katika eneo la vijijini nchini Mali. Anasemekana kuwa wa pili kwa ngazi ya uongozi katika kundi hilo ambalo linapigana na majeshi ya kigeni nchini Mali.
Raia huyo wa Algeria anatuhumiwa kwa mauaji ya mateka wawili kutoka nchi za magharibi Edwin Dyer raia muingereza mwaka 2009 Michel Germaneau raia wa ufaransa mwaka uliofuata. Mwandishi wa BBC Thomas Fessy anasema kuwa ikiwa wataweza kuthibitisha kifo hicho, maswali bila shaka yataibuka kuhusu mateka wa Ufaransa wanaoaminika kuwa walikuwa mikononi mwa Abou Zeid.
Mwezi Januari, Ufaransa ilituma wanajeshi 3,500, Kaskazini mwa Mali, kwa lengo la kuwaondoa wanamgambo wa kiisilamu waliokuwa wameteka sehemu ya jangwa la Sahara.