Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » LIL WAYNE ATOLEWA ICU

LIL WAYNE ATOLEWA ICU

tangazo

Baada ya kukaa kwa takriban siku 6, hatimaye Lil Wayne ametolewa kwenye chumba cha wagonjwa mahututi kwenye hospitali aliyolazwa ya Cedars-Sinai jijini Los Angeles baada ya madaktari kuona kuwa afya yake imekaa vizuri kiasi.
img-lil-wayne-cover_17135846584
Vyanzo vilivyo karibu na Weezy vimeuambia mtandao wa TMZ kuwa kwa sasa Lil Wayne yupo kwenye chumba cha kawaida kwenye hospitali hiyo na hahitaji tena uangalizi wa karibu kama awali baada ya kuoverdose madawa ya kupunguza maumivu wiki iliyopita.

Lil Wayne amekaa ICU tangu Jumatano ya wiki iliyopita.Kwa sasa Lil Tunechi mwenye miaka 30 anasemekana kutembea mwenyewe lakini akiwa amezungukwa na timu ya mabodyguard. Pia anakula mwenyewe na anaweza kuruhusiwa hospitalini hapo siku chache zijazo.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger