Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » RAIS WA VENEZUALA AFARIKI DUNIA....

RAIS WA VENEZUALA AFARIKI DUNIA....

tangazo


Mamia ya wavenezuela walikusanyika mbele ya hospitali ambapo kiongozi wao Hugo Chavez alifariki jana kutokana na ugonjwa wa kansa.



Miongoni mwao walionekana wakipepea bendera za Venezuela huku wengine wakiwa na mabango yenye maandishi, “People, Chavez and revolution, the battle continues”, na kusikika watamka “Chavez lives”. Rais huyo amefariki akiwa na umri wa miaka 58.

Kutokana na kifo hicho, serikali imetenga siku saba za maombolezo ya kitaifa. Wananchi wengi wamekusanyika kwenye maeneo ya wazi kwenye mji mkuu Caracas na miji mingine wakiimba wimbo wa taufa, wakibubujikwa na machozi na kushika picha za kiongozi huyo.

“Asingefariki. Alikuwa rais bora kuwahi kutokea Venezuela,” alisema Frank Aponte, 45, aliyekuwa kwenye mtaa mmoja wa Caracas. Shughuli za kuuaga mwili huo mbele ya viongozi wengine wa kimataifa zitafanyika Ijumaa.

Katiba ya nchi hiyo inasema uchaguzi lazima ufanyike ndani ya siku 30 tangu kifo cha rais lakini serikali bado haijatangaza tarehe.

TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger