Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » WATU WATATU WAMEFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUMTUSI SPIKA WA BUNGE

WATU WATATU WAMEFIKISHWA MAHAKAMANI KWA TUHUMA ZA KUMTUSI SPIKA WA BUNGE

tangazo

Watu watatu wamefikishwa mahakamani katika mikoa ya Kilimanjaro, Dodoma na Mkoa mpya wa Simiyu kwa tuhuma za kutumia lugha za matusi na uchochezi dhidi ya Spika wa Bunge la Jamhuri yak Muungano wa Tanzania.
 
Mkurugenzi wa idara ya habari maelezo ASSAH MWAMBENE ameiambia Clouds Fm kwamba watu wawili walikamatwa kwa tuhuma za kumtumia ujumbe mfupi wa maneno wenye lugha za matusi na mmoja alikamatwa na DVD yenye picha za kuhamasisha lugha za matusi kwa spika wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania ANNE MAKINDA.

  Mapema mwezi uliopita spika MAKINDA alipokea ujumbe mara 400 kwa njia ya simu ya mkononi, pamoja na kupokea simu zote zikiwa na lugha yak matusi, kufuatia namba ya spika kutangazwa hadharani katika mkutano wa chama kimoja cha siasa hapa nchini.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger