Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » , » JOHARI AGIOMA KUTINGISHA MAUNO YAKE MBELE YA RAY

JOHARI AGIOMA KUTINGISHA MAUNO YAKE MBELE YA RAY

tangazo

MKONGWE kwenye ‘Industry’ ya Filamu Bongo, Blandina Chagula ‘Johari’ alitoa kali ya aina yake baada ya kukataa kuzungusha nyonga mbele ya mwigizaji mwenzake, Vincent Kigos ‘Ray’ anayedaiwa ni mpenzi wake

Tukio hilo lililonaswa na mwandishi wetu juzikati, lilitokea katika Viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar wakati wasanii hao walipojumuika pamoja kwa ajili ya kumbukumbu ya mwaka mmoja tangu kitokee kifo cha msanii mwenzao, Steven Kanumba.

Akiwa viwanjani hapo, Johari aliitwa kupanda jukwaani na wasanii wenzake kwa ajili ya kucheza sebene kidogo lakini yeye alikataa na mwandishi wetu alimsikia akijitetea kuwa hawezi kukata nyonga mbele ya wasanii wenzake hususan Ray ambaye ni bosi mwenzake kwenye kampuni yao ya RJ Company.

“Siwezi kujidhalilisha mbele ya umati huo kwa kukata kiuno tena na bosi mwenzangu yupo pale, labda ningekuwa nimelewa kiasi cha kutojitambua hapo ningefanya madudu kama hayo,” alisema Johari.

GPL
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger