Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » KADA WA CHADEMA ATIWA MBARONI KWA KOSA LA KUM MWAGIA TINDIKALI NDUGU MUSA WAKATI WA UCHAGUZI WA IGUNGA

KADA WA CHADEMA ATIWA MBARONI KWA KOSA LA KUM MWAGIA TINDIKALI NDUGU MUSA WAKATI WA UCHAGUZI WA IGUNGA

tangazo
MUSA TESHA  BAADA  YA  KUMWAGIWA  TINDIKALI
 -------------
Kada maarufu wa CHADEMA Shinyanga mjini,Bwana Oscar Kaijage,Jumamosi alikamatwa na askari polisi na kuzuiwa kituo cha kati na jana Jumatatu alisafirishwa kwenda Tabora na kukabidhiwa kwa askari wa huko.

Sababu kuu ya kukamatwa,ni kuhusishwa na tukio la kumwagiwa tindikali Bwana Musa Tesha 9 Sept,2011 huko Igunga kwenye kampeni za uchaguzi mdogo wa Mbunge ambapo mgombea wa CCM bwana Peter Kafumu alimshinda mgombea wa CHADEMA bwana Joseph Kashinde.


Bwana Oscar alifuatwa dukani kwake stand ya mabasi ya  Shinyanga mjini mnamo saa 9 mchana  na askari nane ambao hawakuvaa sare.


Baada ya mazungumzo ya muda mfupi askari hao waliwaomba majirani wa duka hilo wasogee  ili wawe mashuhuda  wakati wanampekua.


Hata hivyo,polisi  hao hawakukuta kitu chochote walichokihitaji na kuamua kuondoka naye kwenda kumpekua nyumbani kwake ambako nako pia hawakuambulia kitu.


Taarifa iliyopatikana  jana  mchana  kutoka ofisi ya RPC shinyanga ni kuwa Oscar amepelekwa Tabora kwenda kufunguliwa mashitaka.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger