Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » SPIKA WA BUNGE AWAVAA WABUNGE "WANAOTUMIA MATUSI" BUNGENI

SPIKA WA BUNGE AWAVAA WABUNGE "WANAOTUMIA MATUSI" BUNGENI

tangazo

Akiongea kwa uchungu , Spika wa Bunge bi Anne Makinda amewashambulia wabunge  leo asubuhi na kuwaambia suti zao walizovaa haziendani na matusi  yanatoka  katika vinywa vyao  ambayo yeye ameshindwa kuyataja kutokana kwa  madai  kuwa mdomo  wake hauwezi kutamka matusi hayo.....

Makinda amesema matusi ndiyo yamekuwa yakitawala katika midomo ya wawakilishi hao na kuacha hoja inayojadiliwa hewani....
 
Spika wa bunge amekwenda mbali zaidi na kuwaambia wabunge hao kwamba hataangalia chama endapo mbunge atavunja kanuni za bunge kwa kuwa kanuni za bunge zinampa nafasi ya kuita polisi na kuja kumchukua mbunge huyo kwa hatua za kisheria.

Makinda  amesema ametumiwa sms ambayo mtumaji amedai hatokaa tena na familia yake kuangalia bunge labda ajifungie chumbani.
 

TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger