tangazo
Kupitia safari redio mtwara,Kamanda wa polisi mkoani Mtwara alisikika akitoa tahadhari kwa wananchi wenye hasira kali dhidi ya mustakabali wa suala la gesi na nia ya serikali kwa maendeleo ya watu wa kusini...
Licha ya serikali kutumia gharama nyingi kuendesha kipindi cha BARAGUMU
LA MSIMBATI kupitia kituo chake cha habari cha TBC ambacho katika
kipindi hiki ni kama nyenzo ya kutoa elimu kwa wananchi wa tanzania
hususani KUSINI , wananchi hao wameonekana kutoelewa na kutokubaliana moja
kwa moja na serikali....
Wananchi manispaa ya Mtwara Mikindani wameaswa kununua mahitaji yao ya
umuhim na kuweka ndani kwa siku ya leo kwani kwa siku ya kesho huduma za
kijamii zitasimama ama zisipatikane moja kwa moja....
Kuna uwezekano mkubwa
wa maduka mbali mbali ya vyakula,masoko,usafiri wa umma kama dala
dala,boda boda na bajaji kusitisha huduma kutokana na TAMKO la
wanaharakati na wakereketwa wa gesi na mustakabali wa mtwara na kusini
ya kwamba huduma hizo kesho zisimame na watu wawe macho kufuatilia
mjadala wa hotuba ya waziri wa nishati na madini BUNGENI na iwapo
hawataona la maana kwenye hotuba hiyo basi wataamua lao la kufanya...
Wanamshangaa RPC kukimbilia SAFARI RADIO kutoa tamko hilo kwani wao hawajapanga kufanya vurugu za aina yoyote zaid ya kutaka haki itendeke
Wanasema kwa kuwa serikali ya CCM imeamua kutumia ubabe basi na wao wataonesha ya upande wao kwa MASLAHI YA VIZAZI VYAO VIJAVYO...
Wanamshangaa RPC kukimbilia SAFARI RADIO kutoa tamko hilo kwani wao hawajapanga kufanya vurugu za aina yoyote zaid ya kutaka haki itendeke
Wanasema kwa kuwa serikali ya CCM imeamua kutumia ubabe basi na wao wataonesha ya upande wao kwa MASLAHI YA VIZAZI VYAO VIJAVYO...

