SHEHA WA TOMONDO- ZANZIBAR AMWAGIWA TINDIKALI
tangazo
Sheha
wa Tumondo Mohamed Omary Said,amemwagiwa tindikali na mtu asiyejulikana
na hivyo kupata maumivu makali sehemu yake ya kifua na jicho kuumia
pia.
Sheha huyo alikimbizwa katika Hospitali ya Mnazi mmoja mjini Unguja ambapo alipatiwa matibabu ya dharura.
Kamanda wa polisi wa Mkoa wa Mjini Magharibi,Mukhadam Khamis,amesema
chombo kilichotumika kumwagia tindikali Sheha huyo kilipatikana eneo la
tukio na kwamba polisi imekichukua kwa kukichunguza kitaalam ili
kugundua aliyekuwa akikitumia kwa kuangalia alama za vidole.
Sheha huyo alimwagiwa tindikali jana usiku wakati alipotoka nje ya
nyumba yake kuchota maji na ndipo mhalifu huyo alipomwagia tindikali na
kwamba hakuweza kumtambua.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK