Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » , » VIGOGO WA DUBAI WAMGOMBANIA LULU MICHAEL ....

VIGOGO WA DUBAI WAMGOMBANIA LULU MICHAEL ....

tangazo

HABARI zilizonaswa na mwandishi  wetu  zinaeleza kuwa nyota wa sinema Bongo, Elizabeth Michael ‘Lulu’, ameitwa katika Jiji la Dubai, Falme za Kiarabu kwa ajili ya kula  bata ikiwa ni pole yake kwa kusota Gereza la Segerea kwa karibu mwaka mmoja.

Chanzo kimoja  kilipenyeza habari kuwa mapedeshee hao wamemualika staa huyo huku ikinyetishwa kwamba, vigogo wa sanaa hiyo Bongo, Steven Mengere ‘Steve Nyerere’ na Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’ ndiyo watakaomsindikiza.
 

“Mapedeshee wamemtumia mamilioni ya fedha Lulu, wanataka kufanya naye pati ya pamoja kwa vile ni miongoni mwa mastaa wa Bongo wanaokubalika nchini humo na pia kumpa pole kwa kukaa gerezani muda mrefu.
 

“Mbali na sherehe hiyo, watakapokuwa nchini humo wanatarajia kuendeleza filamu ambayo wameanza kuirekodi hapa Bongo,” kilisema chanzo hicho.
 

Hata hivyo, chanzo kiliweka wazi kwamba kwa sasa, Lulu si rahisi kusafiri nje ya Bongo kwa vile kesi aliyonayo ina mipaka ya sehemu za kwenda.
Alipotafutwa Dk. Cheni juu ya ishu hiyo, alisema waliomuita Lulu si mapedeshee bali ni Wabongo waishio kule, lakini masharti ya kesi yake hawezi kusafiri nje ya Tanzania.
Dk. Cheni akaulizwa kuhusu yeye na Steve Nyerere kuwepo kwenye safari hiyo ambapo alisema hana ufafanuzi zaidi, akakata simu.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger