Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » "KAMA NINGEKUWA RUGE NINGEMPIGIA MAGOTI LADY JAYDEE NA KUMUOMBA MSAMAHA"....SEBO WA MAGIC FM

"KAMA NINGEKUWA RUGE NINGEMPIGIA MAGOTI LADY JAYDEE NA KUMUOMBA MSAMAHA"....SEBO WA MAGIC FM

tangazo

Katika kipindi cha Sun Downer cha Magic FM, mtangazaji huyo amesema kwamba shangwe zilizolipuka mara baada ya Jaydee kutajwa kuwa miongoni mwa wanaowania tuzo ya msanii bora wa kike katika  tuzo za KTMA, ni ishara ya mwanadada huyo kukubalika katika  jamii. 

Mtangazaji huyo amesema kwamba Jaydee ni mwanamke mwenye uthubutu katika  harakati za kuyasaka maisha na kwamba yeyote mwenye nia ya kukwamisha jitihada zake aibu na iwe juu yake. 

Ameongeza kuwa kukubalika kwa mwanadada huyu pia kulidhihirika pale  watazamaji katika tukio hilo walipomshinikiza Meneja wa msanii huyo (Gadna) kutaja kiingilio na tarehe ya maadhimisho ya miaka 13 ya Jaydee katika  uga wa muziki. 

Hivyo, Sebo anaona ni vyema Ruge akajishusha na kumaliza tofauti zake dhidi ya Jaydee.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger