Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » "NAFIKIRIA KUAHIRISHA SHOW YANGU ILA SI KWA KUMUOGOPA MWANAMKE"...MWANA FA

"NAFIKIRIA KUAHIRISHA SHOW YANGU ILA SI KWA KUMUOGOPA MWANAMKE"...MWANA FA

tangazo
MSANII wa muziki wa kizazi kipya nchini Tanzania Mwana FA anafikiria kuahirisha shoo yake ya kesho kufuatia kifo cha msanii mwenzake wa kizazi kipya Langa Kileo, kilichotokea leo  jijini Dar es Salaam.  

Mwana FA anafikiria kuahirisha shoo yake ya kesho iliyopangwa kufanyika katika viwanja vya Makumbusho ya Taifa jijini Dar es Salaam na tayari ameanza kuwasiliana na meneja wake kwa ajili ya hatua hiyo.

Hii itakuwa ni mara ya pili kwa Mwana FA kuahirisha shoo yake, awali ilipaswa kufanyika Mei 31 mwaka huu lakini ikaahirishwa kutokana na kifo cha aliyekuwa msanii mwenzake wa Bongo Fleva Albert Mangwea.


Hata hivyo Mwana FA ametoa tahadhara ya kejeri juu ya hatua hiyo huku akimtupia madongo mhasimu wake mkubwa Mwanadada Lady Jay Dee...

Katika taarifa yake aliyoitupia katika mtandao wa kijamii wa Facebook Mwana FA amesema kwamba:

7 minutes ago via mobile · Like Mwana FA Halisi : "Msiba wa mwana HIPHOP mwenzetu Langa unanifanya nifikirie kuahirisha show ya kesho. Nawasiliana na manager wangu kisha nitawajuza ,but si kwa kumuogopa mwanamke,Let it be clear" 

Habarimpya
 
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger