Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » SAUTI YA SAIDA KAROLI AKITHIBITISHA KUWA NI MZIMA NA HAJAFA KAMA WATU WANAVYODAI....

SAUTI YA SAIDA KAROLI AKITHIBITISHA KUWA NI MZIMA NA HAJAFA KAMA WATU WANAVYODAI....

tangazo

Mwanamuziki mkongwe wa nyimbo za asili nchini Saida Karoli, amezikanusha tetesi zilizoanza kuenea tangu jana kuwa amefariki kwenye ajali ya boti katika ziwa Victoria.

Akiongea kwa simu  leo asubuhi , Saida ambaye baada ya kutumbuiza kwenye tuzo za Kili wiki iliyopita alielekea Makongorosi Chunya mkoani Mbeya, amesema yupo hai na ni mzima wa afya.

“Mungu wangu, mimi niko hai, ndugu yangu, naomba uwaeleze watanzania kwamba Saida ni mzima, hakuna chochote kilichotokea hata mimi mwenyewe nimeshangaa yaani watu wanapiga simu, ni suala la msiba lakini si kweli,” amesema Saida.



Credit: Bongo5
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger