Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » BINTI ANYIMWA KUGOMBEA UONGOZI KWA SABABU NI MZURI KUPITA KIASI

BINTI ANYIMWA KUGOMBEA UONGOZI KWA SABABU NI MZURI KUPITA KIASI

tangazo
 
Msichana mrembo kutoka Iran amejikuta akikosa nafasi ya uongozi katika halmashauri ya jiji lake kwa kuambiwa kuwa yeye ni mzuri sana hivyo amepitiliza sifa za nafasi hiyo.


Nina Siahkali Moradi (27), alikuwa miongoni mwa wagombea katika uchaguzi wa halmashauri ya jiji la Qazvin nchini Iran, ambapo baada ya kura kuhesabiwa alikamata nafasi ya 14. 


Lakini hata hivyo wiki moja baadaye kura zake zilifutwa na kiongozi wa halmashauri ya jiji hilo kwa maneno ya kejeli akimwambia “We don’t want a catwalk model on the council,”
 
Katika uchaguzi huo Nina alipata kura 10,000 na kumfanya akamate nafasi ya 14 kati ya 163, lakini wapinzani wake katika uchaguzi huo walilalamika kuwa Moradi alipigiwa kura kwasababu ni mzuri sana anavutia, pia mdogo.
 
Kwa mujibu wa The Independent, baraza huchukua washindi 13 wa juu na mgombea anayeshika nafasi ya 14 huwekwa kama ‘reserve’.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger