Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » Baadhi ya mambo yanayoendelea ndani ya kikao cha Zitto Kabwe na waandishi wa habari

Baadhi ya mambo yanayoendelea ndani ya kikao cha Zitto Kabwe na waandishi wa habari

tangazo

Aliyekuwa Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema, Dk Kitilia Mkumbo amekiri kwamba alishirikiana na Samson Mwigamba katika kuandaa waraka wa mabadiliko katika Chama hicho, lakini siri hiyo ivuja baada ya Mwigamba kukamatwa na kunyang'anywa Laptop ambayo ilikuwa na wakara mzima.

Dk Kitilia amefafanua kwamba sababu ya yeye kuandaa waraka huo ilikuwa ni kuleta mabadiliko ndani ya Chama hicho. Kwa upande wake Zitto Kabwe anasema kwamba yeye hawezi kuwa chanzo cha Chadema kufa na kamwe hawezi kukivuruga Chadema kwamba ndicho kilicho mlea.
 
"Nilijiunga Chadema nikiwa na miaka 16, hivi sasa nina miaka 37, ningependa siku moja mtoto wangu aje kuwa mwanachadema, kuna tuhuma nyingi sana juu yangu ambayo kimsingi sikuhusika nayo hata kidogo.
 
Tuhuma kubwa iliyochukuwa nafasi kubwa na muda mwingi katika mkutano wa Kamati Kuu,ni tuhuma za Kamati ya Bunge na Hesabu za Serikali kusema kwamba Chadema haijawasilisha hesabu zake kwa CAG, lakini nikaambiwa kwamba nilipaswa kuwatonya viongozi wa Chadema kabla ya kutangaza hadharani hivyo nikaambiwa kwamba nimekidhalilisha Chama".
 
"MImi nikiwekewa chaguo la nchi na Chama nitachagua nchi kwanza si Chama, hivyo nilifanya vile kwa muujibu wa taratibu za kamati yangu"

"Tuhuma nyingine nikaambiwa kwamba mimi ni mnafiki kwa kukutaa kuchukuwa posho za vikao vya bunge"..

"Mimi sitoki Chadema, na wanaotaka nitoke wanitoa kwa njia wanaotaka wao,na nitakuwa wa mwisho kutoka, nimefanya kazi kubwa ndani ya Chadema,ninapotuhumiwa ninaumia, tuache siasa za chuki.

Bado  anaendelea...
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger