Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » Lulu Michael awahamasisha vijana kupima UKIMWI

Lulu Michael awahamasisha vijana kupima UKIMWI

tangazo

Msanii wa filamu nchini Elizabeth Michael aka Lulu amesema vijana wanatakiwa wawe mstari wa mbele katika kujikinga na maambukizi ya virusi vya Ukimwi.
 
Akizungumza na mwandishi wetu jana katika usiku wa Red Ribbon Fashion Galla iliyofanyika Mlimani City jijini Dar es Salaam, Lulu alisema siku ya Ukimwi duniani inatukumbusha kuangalia tumetoka wapi na tunakwenda wapi na kuangalia wangapi wamepoteza maisha kwaajili ya gonjwa la Ukimwi.
 
“Najumuika na Watanzania leo ,siku ya Ukimwi duniani ambayo hufanyika kila mwaka, kwa kuangalia wangapi wamepoteza maisha, pamoja na kuwahamasisha zaidi vijana Wakitanzania kutumia kinga ili kupunguza maambukizi ya virusi vya Ukimwi ambavyo vinapoteza nguvu ya Taifa,” alisema Lulu.
 
Pia Lulu alisema amekuwa akipima Ukimwi mara kwa mara ili kuangalia afya yake,huku akiwashauri vijana kwenda kupima ili kujua afya zao.
 
“Nimekuwa nikipima HIV kila mara katika hatua za maisha yangu,kuangalia kuhakikisha najiweka katika usalama wa afya yangu,pamoja na kupanga matarajio ya maisha.Sio kuwa ukipima ukagundulikana una HIV utashindwa kupanga malengo yako hapana! ukipata ushauri nasaha, ukajua uishi vipi kwa kuboresha afya yako, maisha yataendelea kama kawaida. Kwahiyo kinachotakiwa vijana ni kujua afya zetu mapema”
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger