Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » , » VICENT KIGOSI AWAPA MAKAVU WABAYA WAKE.....

VICENT KIGOSI AWAPA MAKAVU WABAYA WAKE.....

tangazo

INAWEZEKANA ukawa unafanya kazi lakini baadhi ya watu wakawa wanaziponda kwa chuki zao, ambapo msanii anayefanya poa bongo kwenye tasnia ya filamu Vicent Kigosi ‘Ray’, amesema kuwa wapo baadhi ya wasanii wenye tabia hizo na kudai kama wanaziponda kazi zake basi ni wachawi na wanachuki zao.

Mwandishi wetu alitaka kujua tabia hizo kama zipo katika tasnia hiyo, ambapo msanii huyo aliamua kuweka wazi kuwa popote penye mafanikio lazima kuwe na watu nwenye chuki huku akidai kuwa kuna wasanii wanaozichukia kazi zake kwa sababu anafanya vizuri sokoni kuliko wao.


Alisema kuwa mara nyingi watu wenye tabia hizo ni wale wasiyofanikiwa na kazi yao kubwa ni kusambaza ubaya juu ya watu wengine huku muda wao mwingine wakiutumia vibaya badala ya kubuni kazi za kufanya.


“Kuna watu wabaya sana mimi najua kuna baadhi ya wasanii ambao nipo nao karibu wanazichukia kazi zangu hasa pale zinapoenda sokoni, sijali na ndiyo maana nazidi kubuni kazi nzuri kila kukicha,” alisema.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger