Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » HALI YA MKURUGENZI WA UPELELEZI WAMAKOSA YA JINAI, ROBERT MANUMBA BADO NI MBAYA....HIVI SASA ANAPUMULIA MASHINE

HALI YA MKURUGENZI WA UPELELEZI WAMAKOSA YA JINAI, ROBERT MANUMBA BADO NI MBAYA....HIVI SASA ANAPUMULIA MASHINE

tangazo

HALI ya afya ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai nchini (DCI), Robert Manumba ambaye hivi sasa anapumua kwa msaada wa mashine, bado inahitaji uangalizi wa karibu wa madaktari na wauguzi.

Mkurugenzi wa Tiba wa Hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam, Jaffer Dharsee alithibitisha hayo jana katika taarifa yake iliyoelezea hali ya Manumba anayeendelea kupatiwa matibabu katika hospitali hiyo.

“Uongozi wa hospitali ya Aga Khan unapenda kuujulisha umma, kwamba DCI Manumba bado yuko hospitali anaendelea na matibabu. Hali ya afya yake bado inahitaji uangalizi wa karibu wa madaktari na wauguzi,” alisema.

Katika hatua nyingine, ndugu, jamaa, marafiki na maofisa wa ngazi mbalimbali wa Polisi waliendelea kufika hospitalini hapo kumjulia hali Manumba ambaye amelazwa katika chumba cha wagonjwa wanaohitaji uangalizi maalumu (ICU).

DCI Manumba aliugua ghafla na kulazwa katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) Januari 14, kabla ya kuhamishiwa Aga Khan kwa ajili ya uchunguzi zaidi na kulazwa ICU.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger