tangazo
Idadi
ya vifo vya Waethiopia waliokamatwa Machi mosi, mwaka huu, katika
maeneo ya Kitumbi Barabara ya Segera-Chalinze wakiwa ndani ya makontena
wakisafirishwa kutoka jijini Arusha kuelekea jijini Dar es Salaam
imefikia watano hadi sasa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, COSTANTINE MASSAWE amesema wahamiaji hao walikamatwa baada ya polisi kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema na walikutwa mmoja akiwa amefariki dunia kwa kukosa hewa huku saba wakiwa hawajitambui.
Kamanda MASSAWE, amesema wahamiaji hao ambao wako 54 walichanganywa na mzigo wa Nondo na baada ya magari yaliyowabeba kukamatwa madereva wa magari hayo mawili walitokomea kusikojulikana wakihofia kukamatwa ambapo hadi sasa majina yao hayajatambulika.
Aidha Kamanda MASAWE, ameiomba jamii kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa kuhusiana na vitendo vya aina hiyo ili viweze kudhibitiwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, COSTANTINE MASSAWE amesema wahamiaji hao walikamatwa baada ya polisi kupata taarifa kutoka kwa wasamaria wema na walikutwa mmoja akiwa amefariki dunia kwa kukosa hewa huku saba wakiwa hawajitambui.
Kamanda MASSAWE, amesema wahamiaji hao ambao wako 54 walichanganywa na mzigo wa Nondo na baada ya magari yaliyowabeba kukamatwa madereva wa magari hayo mawili walitokomea kusikojulikana wakihofia kukamatwa ambapo hadi sasa majina yao hayajatambulika.
Aidha Kamanda MASAWE, ameiomba jamii kuendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kwa kutoa taarifa kuhusiana na vitendo vya aina hiyo ili viweze kudhibitiwa.