tangazo
Jukwaa
la Wahariri Nchini TEF, leo limekutana katika kikao chake cha dharura
kilichowashirikisha wahariri kutoka vyombo mbalimbali vya habari, ambapo
kwa pamoja wamekubaliana Kuunda timu ya watu watano kwa ajili ya
kufanya utafiti wa kihabari wa tukio la kutekwa, kupigwa na kujeruhiwa
kwa Mwenyekiti wa TEF Absalom Kibanda.
Amesema timu hiyo itaundwa na wajumbe watatu kutoka TEF na mjumbe mmoja mmoja kutoka Baraza la Habari Tanzania (MCT) na Taasisi ya Vyobo vya Habari Kusini mwa Afrika – Tawi la Tanzania (Misa – Tan), na kwamba Timu hiyo itaanza kazi katika muda wa wiki moja kuanzia sasa na itafanya kazi hiyo kwa wiki mbili.


