Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » OMBA OMBA WATAFUTIWE SULUHISHO LA KUDUMU...

OMBA OMBA WATAFUTIWE SULUHISHO LA KUDUMU...

tangazo
Ndugu watanzania wenzangu, Inasikitisha  sana  kuwaona ombaomba wengi katika  maeneo  mengi  ya  dodoma na  eneo la Ubungo mkoani Dar es salaam na maeneo mengine ya mikoani wakiwa katika maeneo hayo kila siku. ..



Pamoja na kuwasaidia fedha kidogo msaada huo hautoshi kuwaondoa pale walipo kutokana na hali zao za kutokuwa na uwezo wa kufanya kazi za kutumia nguvu.

Wakati serikali yetu ikipitisha bajeti zenye kutumia fedha nyingi kwa kulipana posho na mishahara minono kwa watumishi wa ngazi za juu hasa wabunge na mawaziri inatakiwa pia kuwakumbuka walemavu wale wasio na msaada wowote wa kuwafanya waishi kama watanzania wegine kwa kuwaanzishia vituo maalumu ambapo watapata huduma na kutunzwa ..

 
Naomba ndugu wananchi na wabunge tuishinikize serikali ili iweze kulifanyia kazi swala hili kwani hawakupenda kukaa chini na kunyeshewa na mvua wakiomba msaada.


TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger