Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » WANAFUNZI WA CHUO CHA UHASIBU WALIOKUWA WAMEFUKUZWA WAMETAKIWA KUTUMA MAOMBI UPYA

WANAFUNZI WA CHUO CHA UHASIBU WALIOKUWA WAMEFUKUZWA WAMETAKIWA KUTUMA MAOMBI UPYA

tangazo


Kutokana na Chuo kufungwa, Baraza la Uongozi wa Chuo
katika kikao chake cha dharura cha tarehe 03 Mei 2013
kimeagiza wanafunzi wote kuanzia ngazi ya Cheti mpaka
Stashahada ya Uzamili kuzingatia yafuatayo:
 
1. Kila Mwanafunzi anatakiwa kutuma maombi mapya ya
kujiunga na Chuo.
2. Barua ya maombi hayo ipitishwe kwa Mkuu wa Wilaya
anapoishi mwanafunzi. Kwa mwanafunzi wa Stashahada
ya Uzamili ya Uhasibu barua yake ya maombi ipitie kwa
Mhasibu Mkuu wa Serikali.
3. Katika maombi hayo mwanafunzi anaagizwa kueleza
namna alivyoshiriki katika vurugu za tarehe 24 Aprili
2013.
4. Mwanafunzi awe amekamilisha malipo ya ada iliyobaki
wakati anatuma maombi yake.
5. Mwisho wa maombi ni tarehe 16 Mei 2013.
Maombi yapelekwe kwa anwani ifuatayo:
Mkuu wa Chuo,
Chuo cha Uhasibu Arusha
S. L. P. 2798
Arusha.
08 Mei 2013
TEMBELEA TOVUTI YA CHUO
www.iaa.ac.tz
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger