Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » NAPE AKWEPA KUZUNGUMZIA MATOKEO UDIWANI ARUSHA..."WAULIZENI VIONGOZI WA CCM ARUSHA"

NAPE AKWEPA KUZUNGUMZIA MATOKEO UDIWANI ARUSHA..."WAULIZENI VIONGOZI WA CCM ARUSHA"

tangazo

Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi na Uenezi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye

Katibu wa Halmashauri Kuu (NEC), Itikadi na Uenezi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Nape Nnauye, amesema wanaopaswa kuulizwa jambo lolote linalohusu uchaguzi wa udiwani wa kata nne uliofanyika Jumapili wiki iliyopita, jijini Arusha, ni viongozi wa chama wa mkoa huo.

Nape alisema hayo alipozungumza na Nipashe  jijini Dar es Salaam jana, baada ya kutakiwa kutoa maoni yake kufuatia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kuibuka mshindi katika kata zote nne.

“Waulize wenyewe. Siwezi kuzungumzia issue (suala) ndogo. Unajua chama chetu kimegawa majukumu. Kule kuna mwenyekiti wa mkoa, katibu pamoja na wengineo,” alisema Nape.


Alipoulizwa sababu  za kutoa maoni katika chaguzi nyingine mara tu matokeo yanapotangazwa, kama vile Jimbo la Igunga, Nape alisema uchaguzi huo unahusu ubunge  tofauti na udiwani.

Alisema hata katika uchaguzi wa kata nyingine 22, alizungumza kwa kuwa ulikuwa umehusisha kata mbalimbali nchini na siyo mkoa mmoja.

TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger