Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » CLINTON AMPONGEZA RAIS KAGAME.....ANADAI KUWA TUHUMA DHIDI YAKE HAZIJATHIBITISHWA MAHAKAMANI

CLINTON AMPONGEZA RAIS KAGAME.....ANADAI KUWA TUHUMA DHIDI YAKE HAZIJATHIBITISHWA MAHAKAMANI

tangazo

Aliyekuwa rais wa marekani Bill Clinton amempongeza rais wa Rwanda Paul Kagame kwa  mafanikio ya  nchi yake  licha ya madai kwamba amekuwa akiunga mkono makundi ya waasi katika Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambayo yanakiuka haki za kibinadamu.

Bwana Clinton amesema katika mahojiano na BBC kwamba madai hayo ambayo Rwanda inayakataa hayajathibitishwa mahakamani.
 
Pia alisema kuwa kuna changamoto kubwa katika mpaka wa Rwanda na Congo, kwani una watu chungu nzima ambao walihusika na mauaji ya halaiki miaka ya tisini.
 
Lakini bwana Clinton amesema kuwa anathamini serikali ya Rwanda kutokana na mafanikio ya kiuchumi yalioafikiwa chini ya rais Kagame.
 
Kiongozi huyo amekuwa akizuru mataifa ya Afrika pamoja na mwanawe Chelsea ili kujionea miradi ya wakfu wake.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger