Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » Baba afikishwa mahakamani baada ya kumbaka mwanae

Baba afikishwa mahakamani baada ya kumbaka mwanae

tangazo
MKAZI wa Kijiji cha Njoro wilayani Kiteto mkoani Manyara, Mohamed Ally (42) amefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi kwa tuhuma za kumbaka mtoto wake wa kufikia. 

Mwendesha Mashitaka wa Polisi, Paulo Kimaro alidai mahakamani kuwa tukio hilo lilitokea Septemba 9 mwaka huu nyumbani kwa mtuhumiwa huyo alipombaka mtoto huyo, mwanafunzi wa darasa la saba.
 

Alidai siku hiyo mke wake alitoka na aliporejea kutaka kuingia ndani alisukumwa nje na baada ya kulazimisha kuingia ndipo akagundua kuwa mumewe alikuwa anafanya mapenzi na mtoto wake huyo

Kimaro alidai kutokana na hali hiyo aliomba msaada ofisi ya kijiji cha Njoro na mtuhumiwa akakamatwa na kufikishwa polisi na baadaye mahakamani.

Mtuhumiwa alikana mashitaka na alirejeshwa rumande hadi Septemba 23 mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.

Mke wa mtuhumiwa, Salima Hamisi aliiambia mpekuzi blog kuwa mwanafunzi huyo ni mtoto wa kulea na walimchukua akiwa na umri wa miaka miaka minne.

Kwa mujibu wa taarifa mwanafunzi huyo alifanya mtihani wa taifa wa darasa la saba kwa siku ya pili jana.

TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger