Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » Mtuhumiwa ALIYEJINYEA mahakamani wakati akisomewa mashitaka yake afungwa miezi sita jela jijini DAR.

Mtuhumiwa ALIYEJINYEA mahakamani wakati akisomewa mashitaka yake afungwa miezi sita jela jijini DAR.

tangazo
 
Mtu mmoja amehukumiwa kifungu cha miezi sita jela katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Sokoine Drive kwa kosa la kujisaidia haja kubwa ndani ya Mahakama wakati akisomewa mashitaka. 

Adhabu hiyo ilitolewa papo hapo baada ya mshitakiwa Hassan Omary (25) kufanya kitendo hicho aliposomewa mashitaka mengine tofauti.
 
Hakimu William Mutaki ndiye aliyetoa hukumu hiyo. Wakati akisomewa mashitaka sanjari na washitakiwa wengine watatu ya kubughudhi abiria maeneo ya Kariakoo, Omary inadaiwa alitokwa haja kubwa.
 
Mwandishi alishuhudia mshitakiwa huyo akisafisha eneo la mahakamani alikochafua kabla ya kupelekwa jela. Wengine anaoshitakiwa nao katika kesi hiyo ni Mohamedi Mussa (20),Hassani Ramadhani (18),Shukuru Adison (26) na Ally Omary (28).

Mwendesha mashitaka wa serikali John kijumbe alidai mbele ya Hakimu Mfawidhi William Mutaki kuwa washitakiwa walitenda kosa la kuwanyanyasa na kuwabugudhi abiria ,Septemba 18 ,mwaka huu Kariakoo, jijini Dar es Salaam. Washitakiwa wengine walirudishwa rumande hadi Oktoba 2,mwaka huu kesi hiyo itakapotajwa tena.
 
Katika kesi nyingine, mshitakiwa Jacob Sasita (28) amehukumiwa kifungo cha mwezi mmoja baada ya kukiri kuwanyanyasa abiria .
 
Sasita alikuwa miongoni mwa washitakiwa saba waliofikishwa mahakamani kwa kosa hilo. Washitakiwa wengine ni Ramadhani Juma (38),Abeid Ismail (25),Abuu Rajabu(25),Salimu Kijimbo (39),Ally Hassani (28),Josephb Chambo (29)na Fabiani Thomas (28) ambao walikana kutenda kosa baada ya kusomewa mashitaka.
 
Mbele ya Hakimu Mkazi Timoth Lyon, Mwendesha Mashitaka wa Serikari, Richard Magudi alidai watu hao walitenda kosa la kuwanyanyasa abiria katika kituo kikuu cha mabasai cha Ubungo ,kabla ya kukamatwa na askari polisi. Walirudishwa rumande hadi Oktoba 2 mwaka huu kesi itakapotajwa tena.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger