Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » NGEDERE ATIMUKA NA BUKTA YA BEKI WA TIMU YA SIMBA....

NGEDERE ATIMUKA NA BUKTA YA BEKI WA TIMU YA SIMBA....

tangazo
 
 Ngedere mmoja kwa jina la Sharobaro amekuwa kivutio katika kambi ya Simba iliyopo kwenye Fukwe za Bamba nje kidogo ya Jiji la Dar, eneo la Kigamboni, ambapo gazeti la Championi Jumatano lilimshuhudia ngedere huyo akivinjari katika vyumba vya wachezaji wa timu hiyo na kucheza na beki wa kikosi hicho, Issa Rashid ‘Baba Ubaya’ lakini baadaye akakimbia na bukta ya mazoezi ya nyota huyo.

Mara baada ya ngedere huyo kuchukua bukta hiyo na kukimbia nayo kwa umbali mfupi, Baba Ubaya alimfukuza huku akimuita kwa jina la Sharobaro ambapo aliiachia chini, kisha kumrukia mguuni na kurudi katika varanda ya chumba chake.

Baba Ubaya aliliambia gazeti hilo kuwa, ngedere huyo ni rafiki yake mkubwa na aliichukua bukta hiyo katika michezo yao na hana tabia ya kung’ata watu kama ilivyo kwa wengine: “Huyu ni rafiki yangu mkubwa, anacheza na wengi lakini mimi ndiyo kanizoea zaidi,” alisema Baba Ubaya. 


TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger