Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » Ajali ya pikipiki yaua wawili jijini Mwanza....Tunaomba radhi kwa picha.

Ajali ya pikipiki yaua wawili jijini Mwanza....Tunaomba radhi kwa picha.

tangazo

Watu wawili wamefariki dunia papo hapo wilayani Bukombe mkoani Geita wakitumia usafiri wa bodaboda kufuatia pikipiki waliyokuwa wakisafiria kuteleza kwenye mchanga ikiwa kwenye mwendo kasi na kisha kukanyagwa vibaya vichwani na gari aina ya Noah ambayo walikuwa wakipishana nayo.
 
Kwa mujibu wa shuhuda wa tukio hilo,  dereva wa bodaboda ambaye alikuwa na abiria wake mwanamke mwenye mizigo, alikuwa katika mwendo wa kasi. 

Hatua kadhaa kabla ya kupishana na gari hilo, matairi ya pikipiki yake yalishindwa kuhimili mchanga uliopo barabarani ndipo alipokosa uwiano wa kumiliki chombo hicho cha usafiri na kutereza kisha wakaanguka katikati ya barabara.
 
Sekunde chache gari la abiria aina ya Noah ambalo mpaka shuhuda huyo anaondoka kwenye tukio la ajali hakufanikiwa kulinasa namba zake likiwa kwenye kasi liliwapitia vichwani bodaboda na abiria wake ambao walikufa papo hapo.
 

-Gsengo.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger