Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » Polisi wafanikiwa kumkamata kinara wa shambulizi la Dr. Mvungi lililopelekea kifo chake

Polisi wafanikiwa kumkamata kinara wa shambulizi la Dr. Mvungi lililopelekea kifo chake

tangazo

JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linamshikilia John Mayunga (56) mkazi wa Kiwalani kwa tuhuma za kumjeruhi kwa mapanga sehemu za kichwani na usoni, Dk. Sengondo Mvungi.
 
Taarifa hizo zimetolewa ikiwa ni siku moja tangu mwanasheria huyo maarufu kufariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Millpark nchini Afrika Kusini juzi alasiri.

Dk. Mvungi alivamiwa Novemba 3, mwaka huu, saa 6:30 usiku na watu wanaosadikiwa kuwa majambazi, nyumbani kwake Kibamba, Kata ya Mpiji Magohe, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam kisha kujeruhiwa na kuporwa sialaha, kompyuta na fedha.
 
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamishna wa kanda hiyo, Suleiman Kova, alisema askari walipata taarifa kutoka kwa raia wema kwamba Mayunga alishiriki kikamilifu na wenzake katika tukio hilo.
 
Alisema kuwa waliambiwa kuwa mtuhumiwa huyo alikuwa maeneo ya Mtaa wa Twiga Jangwani akiangalia televisheni, ndipo akakamatwa na kuhojiwa ambapo alikubali kuhusika moja kwa moja na tukio hilo.
 
Kova alisema taratibu za upekuzi zilifanyika na katika harakati hizo kwenye chumba anacholala, ilipatikana silaha ambayo ni bastola aina ya Revolver  namba BDN 6111 pamoja na risasi 21 za bunduki hiyo.
 
Vitu vingine vilivyokutwa ni vifaa vya mlipuko/baruti aina ya explogel yenye muundo wa sausage, tambi 2 ambazo ni viwashio vya baruti (detonator) na milipuko 4 ambayo imeunganishwa na tambi tayari kwa kutumia.
 
“Mtuhumiwa Mayunga alipohojiwa kuhusu umiliki wa silaha hiyo  hakuwa na kibali chochote cha umiliki, badala yake alieleza ni kati ya vitu walivyoiba yeye na wenzake nyumbani kwa Dk. Mvungi,” alisema.
 
Alisema kuwa silaha hiyo ilitambuliwa na familia ya marehemu na kwamba ilikuwa chini ya himaya yake. Kwamba kumbukumbu za maandishi zinaonyesha kuwa ni jambazi mzoefu na hivi karibuni alimaliza kifungo cha miaka saba jela kwa makosa ya ujambazi.
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger