Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » , » JACK WOLPER AWAVAA MAPEDESHEE WANAOPENDA KUTUKUZWA

JACK WOLPER AWAVAA MAPEDESHEE WANAOPENDA KUTUKUZWA

tangazo
Kama unakerwa na tabia za mapedeshee wapenda sifa kwa kutajwa kwenye nyimbo za muziki wa dansi na kumwaga hela ukumbini, hauko peke yako. Jacqueline Wolper naye humchefua. 



“Napenda kutumia fursa hii leo kuzungumza kitu fulani kidogo tu ambacho nimekiona mimi,” ameandika Wolper kwenye blog yake. 

“Mara nyingi nimekua nikisikia kwenye nyimbo nyingi za wanamuziki wa Tanzania hata wa maeneo mbali mbali kama Jamhuri ya watu wa Congo wakiwataja watu flani flani ambao inaaminika na watu wenye kipato kikubwa kifedha au huwa wanawasaidia kimuziki hata kimaisha wakati mwingine.

Kinachonishangaza kwanini wanapenda kuwatunza kwenye majukwaa tuu? Hao wanaojiita mapedeshee wanaopenda kutajwa kwenye nyimbo za hao wasanii. Nawaomba mapedeshee waende kwenye vituo vya kulea watoto yatima na kutoa misaada ya kifedha na Inshalah Mwenyezi Mungu atawazidishia.”
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger