Ungana nasi kwa kuandika email yako hapa ili upate habari mpya kupitia email yako bila usumbufu:


Home » » BREAKING NEWS: NDEGE YADONDOKA JIJINI ARUSHA NA KUUA MTU MMOJA

BREAKING NEWS: NDEGE YADONDOKA JIJINI ARUSHA NA KUUA MTU MMOJA

tangazo
Habari zilizotufikia hivi punde ni kwamba ndege iliyokuwa inamilikiwa na Wakili maarufu Marehemu Nyaga Mawala aliyefariki wiki 3 zilizopita na kuzikwa huko Nairobi imeanguka ikiwa katika hatua za mwisho za kutua  katika kiwanja cha ndege cha arusha.

Taarifa zinasema kuwa ndege hiyo ilikuwa na rubani pekee anayejulikana kwa jina la Jamal B S, au maarufu kama Bob Sambeke aliyekuwa anatokea West Kilimanjaro.


Taarifa zaidi zinasema kuwa  rubani huyo   amefariki  muda  mfupi  baada  ya  ajali  hiyo  kutokea  na   mwili  wake  umekimbizwa   hospitali ya Mount Meru
...

Maelezo zaidi kuhusu ajali hiyo ni kwamba ndege hiyo ilijaribu kutua baada ya masaa ya kawaida ya kufunga kiwanja(saa 12.30jioni) kupita.


Kiwanja cha ndege cha Arusha hakina taa za AGL, hivyo huwa kinamaliza au kufunga shughuli zake saa 12.30 za jioni, na hivyo kina'operate kwa masaa 12 tu.Na kawaida ma'controller huondoka baada ya closure ya kiwanja..

Mungu  ailaze  mahali  pema  roho  ya  marehemu
TUPE MAONI YAKO
KAMA UMEGUSWA NA HUDUMA ZETU, TUNAOMBA UUNGANE NASI KATIKA PAGE YETU YA FACEBOOK HAPO CHINI. BOFYA "LIKE" KAMA BADO HUJA LIKE PAGE YETU.
KUMBUKA KU LIKE UKURASA WETU WA FACEBOOK
 
Support : mpekuzi | John mpekuzi | Wataalam
Copyright © 2009. DOMO LANGU - All Rights Reserved
Template designed by mpekuzi
Proudly powered by Blogger